Huruma

Huruma (kutoka neno la Kiarabu) ina maana ya wema ulio tayari kusaidia na kusamehe.[1][2]

Huruma na Ukweli vikiwa pamoja katika mchoro huu mdogo wa karne ya 13 kuhusu Zaburi 85:10.

Sifa hiyo kwanza ni wa "Mungu" kadiri ya dini mbalimbali, zikiwemo Uyahudi,[3] Ukristo[4] na Uislamu.[5]

Katika karne ya 20, iliyojaa ukatili wa vita vingi, sifa hiyo imezingatiwa zaidi katika ibada kwa Huruma ya Mungu.[6][7]

Kutokana na imani hiyo, binadamu pia anapaswa kuwa na huruma na kutekeleza matendo ya huruma ya kiroho na ya kimwili.[8][9][10][11]

Hata katika jamii, huruma inahitajika katika mahusiano yoyote pamoja na haki.[1][2]

Yesu alitangaza (Math 5:7), "Heri wenye huruma, maana hao watapata huruma" (kutoka kwa Mungu).[4][12]

Mara nyingi Liturujia inamlilia Mungu awe na huruma.[13]

Tanbihi

Viungo vya nje

Wikimedia Commons ina media kuhusu:
Makala hii kuhusu mambo ya dini bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu mada hii kama historia yake au uenezi wake?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.