Sentensi

Sentensi ni kundi la maneno ambalo lina kiima na kiarifa na hutoa maana kamili; ndiyo kipashio cha juu kabisa katika tungo.

Aina za sentensi

Makala kuu ya: Tungo sentensi

Kuna aina kuu nne za sentensi nazo ni:

  • Sahili
  • Changamano
  • Ambatano
  • Shurutia

1. Sentensi sahili - Hii ni aina ya sentensi iliyoundwa kwa kishazi huru kimoja tu, mfanoː Mama anakula.

2. Sentensi changamano - Hii ni aina ya sentensi iliyoundwa kwa kishazi tegemezi na kishazi huru, mfanoː Mtoto aliyepotea ameonekana.

3.Sentensi ambatano - Hii ni aina ya sentensi iliyoundwa kwa sentensi mbili zilizounganishwa na kiunganishi, mfanoː Baba analima ingawa mama anakula.

Sentensi ambatano huweza kuundwa kwaːa. sentensi sahili + sentensi sahili.b. Sentensi sahili + sentensi changamano.c. Sentensi changamano + sentensi changamano.

4. Sentensi shurutia - Hii ni aina ya sentensi iliyoundwa kwa mofimu za masharti, mfanoː ki, nge, ngeli pamoja na ngali.Njia za uchanganuzi wa sentensiːa. Njia ya matawi au ngowe.b. Njia ya mishale au mistari. c. Njia ya visanduku au jedwali.d. Njia ya maneno.

Hatua za uchanganuzi wa sentensiː1. Kuainisha sentensi husika2. Kugawa sentensi katika kiima na kiarifu3. Kuonesha vipashio vya kiima na kiarifu4. Kuainisha aina za maneno5. Kuandika sentnsi husika kwa kila panapohusika

Muundo wa sentensi

Sentensi huundwa kwa sehemu kuu mbili:

  • Kiima (K)
  • Kiarifu (A)

Tazama pia

Makala hii kuhusu mambo ya lugha bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Sentensi kama historia yake, uenezi au maendeleo yake?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.