Mileto

Mileto (kwa Kigiriki Μῑ́λητος, Mīlētos) kuanzia mwaka 1000 KK hivi ulikuwa mji wa Wayunani huko Karia kwenye mto Meandro unapoishia katika Bahari ya Kati, kwenye pwani ya Uturuki wa leo, karibu na kijiji cha Balat.

Maghofu ya thieta ya Mileto.

Kabla ya uvamizi wa Wapersia katikati ya karne ya 6 KK ulitajwa kuwa mkubwa na tajiri kuliko miji yote ya Wagiriki.

Maghofu yake ni kati ya mahali muhimu pa akiolojia[1][2][3][4][5][6].

Mtume Paulo alifika huko mwaka 58 akakutana na viongozi wa Kanisa la mji jirani, Efeso (Mdo 20:15–38), ambapo alikaa miaka mitatu na kutoka huko alieneza Ukristo katika mkoa mzima wa Asia (Mdo 19:10, 20; 1Kor 16:9).

Inawezekana alirudi tena huko miaka 65-66 kwa kuwa aliandika kwamba aliacha huko Trofimo (2Tim 4:20), na si katika safari ile ya kwanza (Mdo 21:29).

Tanbihi

Marejeo

  • Gorman, Vanessa B. (2001). Miletos, the Ornament of Ionia: A History of the City to 400 BCE. Ann Arbor, MI: Michigan University Press. ISBN 9780472111992. 

Viungo vya nje

Wikimedia Commons ina media kuhusu:
Makala hii kuhusu maeneo ya Uturuki bado ni mbegu.
Je unajua kitu kuhusu Mileto kama historia yake, biashara, taasisi zilizopo, watu au utamaduni?
Labda unaona habari katika wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.