Tandu
Tandu | ||||||||
---|---|---|---|---|---|---|---|---|
Tandu kichwa-chekundu | ||||||||
Uainishaji wa kisayansi | ||||||||
| ||||||||
Ngazi za chini | ||||||||
Oda na familia:
Oda Lithobiomorpha
Oda Craterostigmomorpha
Oda Scolopendromorpha
Oda Geophilomorpha
|
Tandu ni aina za arithropodi wembamba na warefu katika ngeli Chilopoda ya nusufaila Myriapoda wenye miguu mingi. Wanafanana kijuujuu na majongoo lakini hawa huenda polepole na hula dutu ya viumbehai, viani na kuvu. Tandu huenda mbio na hula wanyama wengine (invertebrati na vertebrati). Hata kama tandu huitwa centipedes (miguu mia) kwa Kiingereza na majongoo huitwa millipedes (miguu elfu), kwa ukweli wana kwa kadiri nambari sawa ya miguu: tandu wana miguu 16 hadi 300 na majongoo 36 hadi 750.
Spishi kadhaa za Afrika
- Lithobius variegatus, Tandu Milia (Common banded centipede)
- Pachymerium ferrugineum, Tandu Mwekundu (Pachymerium ferrugineum)
- Scolopendra abnormis, Tandu wa Kisiwa cha Nyoka (Serpent Island centipede)
- Scolopendra cingulata, Tandu Milia wa Mediteranea (Mediterranean banded centipede)
- Scolopendra morsitans, Tandu Kichwa-chekundu (Red-headed centipede au Tanzanian blue ringleg)
- Scutigera coleoptatra, Tandu wa Nyumbani (House centipede)
Picha
- Tandu milia
- Tandu milia wa Mediteranea
- Tandu wa nyumbani
🔥 Top keywords: Maalum:TafutaMwanzoFasihi simuliziAina za manenoShairiVivumishiMikoa ya TanzaniaOrodha ya makabila ya TanzaniaOrodha ya Mawaziri Wakuu wa TanzaniaUfahamu wa uwezo wa kushika mimbaLughaOrodha ya mikoa ya Tanzania kwa eneoKamusi za KiswahiliMofimuFasihiNembo ya TanzaniaMawasilianoSentensiMarie AntoinetteKamusiMange KimambiKumaViwakilishiAlama ya uakifishajiKitenziFani (fasihi)TamthiliaVitendawiliNominoKiswahiliMaudhuiSilabiTanzaniaJumuiya ya Afrika MasharikiKisaweVieleziYoung Africans S.C.Kiwakilishi nafsiDiamond Platnumz