Anjelo wa Acri

Anjelo wa Acri, O.F.M.Cap. (jina la awali Luca Antonio Falcone, 19 Oktoba 1669 - 30 Oktoba 1739) alikuwa padri wa Acri (Calabria, leo nchini Italia), maarufu kama mhubiri wa Neno la Mungu.[1]

Mchoro wa mwaka 1754.

Papa Leo XII alimtangaza mwenye heri tarehe 18 Desemba 1825[2], halafu Papa Fransisko alimtangaza mtakatifu tarehe 15 Oktoba 2017.

Sikukuu yake huadhimishwa tarehe 30 Oktoba[3].

Maisha

Kabla hajatulia utawani alitoka mara mbili, lakini hatimaye alidumu na kufanya kazi kubwa ya uinjilishaji katika Ufalme wa Sisili mbili[4]akiongoa watu wengi sana, hata akaitwa "Malaika wa Amani" na "Mtume wa Kusini".[5]

Pia alijulikana kwa sababu ya kujaliwa njozi, kutoka nje ya nafsi mara kadhaa wakati wa Misa, na hata kupatikana mahali pawili kwa wakati mmoja.[6][7]

Tanbihi

Viungo vya nje

Makala hii bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Mkristo huyu, kama wasifu wake, habari za maisha au kazi yake?
Je, unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuiongezea habari.