Interahamwe

wanamgambo waliohusika na mauaji mengi wakati wa mauaji ya kimbari ya 1994 Rwanda

Interahamwe ilikuwa kundi la wanamgambo lililoanzisha mauaji ya kimbari nchini Rwanda mnamo 1994. Katika mauaji hayo, takriban milioni moja ya raia, hasa Watutsi lakini pia Wahutu wasiochukiana nao, waliuawa[1][2].

Bendera ya Interahamwe

Interahamwe ilianzishwa mnamo 1990 kama tawi la vijana la National Republican Movement for Democracy and Development (MRND kwa kifupi chake cha Kifaransa).

Interahamwe walifukuzwa Rwanda na jeshi la Rwandan Patriotic Front (RPF) katika vita ya wenyewe kwa wenyewe ya Julai 1994. Wametangazwa kuwa kundi la kigaidi na serikali nyingi za Afrika na kimataifa. Interahamwe na makundi yaliyotokana nayo wanaendelea kupiga vita ya msituni dhidi ya Rwanda kutoka vituo vyao katika nchi jirani.

Mbinu

Interahamwe mara nyingi walitumia mapanga ('mupanga' kwa Kinyarwanda) kwa kutekeleza mauaji, lakini bunduki, mabomu na zana nyingine zilitumika pia.

Marejeo

Makala hii kuhusu mambo ya kihistoria bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Interahamwe kama enzi zake au matokeo yake?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.