Kasri

Kasri ni makazi makuu, ambayo mara nyingi hutumika kama makazi ya kifalme au nyumba ya mkuu wa nchi au mtu mwenye cheo kikubwa, kama vile askofu au askofu mkuu. [1]

Kasri la msimu wa baridi, jumba la kifalme huko Saint Petersburg, Urusi ; ambayo ilitumika kama makazi rasmi ya watawala wa Urusi .

Kasri hutofautishwa na ngome kwa kuwa ngome huwa na kuta za ulinzi.

Kasri za kale

Kasri ya Dario I Persepoli, mji mkuu wa kifalme wa Uajemi

Kasri za kale zajumuisha majumba ya Waashuru huko Nimrud na Ninawi na kasri za Kiajemi zikwemo za Persepoli na Susa.[2]

Afrika

Ethiopia

Katika mji wa Addis Ababa kuna Kasri la Menelik. Ni jumba la kifalme ambalo kwa sasa linatumika kama makazi ya waziri mkuu wa Ethiopia. Ndani ya eneo hilo kuna makanisa machache, makaburi na nyumba za watawa. Hapo awali, ilitumika kama makazi ya wafalme wa Ethiopia.

Nigeria

Kasri ya amiri wa Emirati ya Bauchi nchini Nigeria

Kasri la Olowo, mtawala wa ukoo wa Yoruba Owo wa Nigeria, inakubaliwa kuwa kasri kubwa zaidi Afrika nzima. Inajumuisha nyua zaidi ya 100, kila moja ikiwa na matumizi ya kipekee ya kitamaduni.

Katika Jimbo la Kano la Nigeria, Gidan Rumfa hufanya kazi kama makazi ya Amiri wa Kano tangu karne ya 15 ilipojengwa.

Katika Jiji la Benin, mji mkuu wa Jimbo la Edo, kuna Kasri la Oba wa Benin. Inatumika kama nyumba ya Oba wa Benin, ambaye ni mtawala wa jadi wa waedo. Kasri ya sasa ni ujenzi mpya uliofanyika chini ya uongozi wa Eweka II baada kasri ya awali kubomolewa mnamo 1897 na Waingereza.

Rwanda

Kasri asili ya Mfalme Nyanza nchini Rwanda

Rwanda ina kasri tatu. Huko Nyanza, mji mkuu wa zamani wa Ufalme wa Rwanda, kuna kasri mbili. La kwanza ni kasri la Mfalme wa kitamaduni ambalo limejengwa kwa mtindo wa kienyeji na yalikuwa makazi ya mfalme wa Rwanda. Kasri la pili la mfalme lililopo Nyanza limejengwa kwa mtindo wa kisasa zaidi. Kasrila tatu liitwalo Kasri la Rwesero, lilijengwa kwa ajili ya Mutara III, lakini alikufa kabla ya kukamilika kwake. Kasri hiyo imegeuzwa kuwaJumba la Makumbusho la Sanaa la Rwesero .

Uganda

Kasri ya Makabaka ya Ufalme wa Buganda ni eneo maarufu inayojulikana katika mji mkuu wa Kampala.[3]

Asia

Mji haramu huko Beijing nchiniChina

Brunei

Istana Nurul Iman ni moja ya kasri kubwa duniani na ni makazi rasmi ya sultani wa Brunei, Hassanal Bolkiah na makao makuu ya serikali ya Brunei.[4] Kasri inapatikana kilomita chache kusini mwa Bandar Seri Begawan,

China

Mfano mashuhuri wa makasri ya Kichina ni Mji haramu, kasri kifalme la Milki ya China kutoka kwa nasaba ya Ming (tangu Mfalme Yongle ) hadi mwisho wa nasaba ya Qing. Ipo Beijing, ndiyo kasri kubwa zaidi lililopo duniani kwa sasa.[5] [6] [7] Mfano mwingine ni Kasri la Majira ya joto lililoko katika kitongoji cha kaskazini mwa Beijing na Kasri la Mukden huko Shenyang.

Mandahri ya Kasri la Kifalme la Shenyang

Uturuki

Kasri la Topkapi, Istanbul

Kasri la Topkapi huko Istanbul lilianza mnamo mwaka 1459, na lilibadilishwa kuwa jumba la kumbukumbu mnamo mwaka 1923. Ilikuwa kitovu cha serikali na vile vile makazi ya Makhalifa wa Milki ya Osmani.

Kufikia karne ya 19 Topkapı iliachwa kama makazi na badala yake Kasri jipya la Dolmabahçe na Kasri la Yıldız zilitumika.

Angalia pia

Marejeo