Maabadi

Maabadi ni mahali popote pa kufanyia ibada, kama vile hekalu, kanisa, msikiti, patakatifu n.k.

Pia tunaweza kusema ni sehemu iliyowekwa wakfu au ni eneo maalum lililojengwa ambalo mtu au kundi la watu kama vile kusanyiko hukutana kufanya ibada au kujifunza masomo ya kidini. Jengo lililojengwa kwa lengo hili wakati mwingine huitwa nyumba ya ibada.

Chini ya Sheria ya Kimataifa ya Kibinadamu[1] na Mikataba ya Geneva[2] nyumba za ibada hupewa ulinzi maalum sawasawa na ulinzi unaotolewa kwa hospitali kwa kuonyesha msalaba mwekundu.

Marejeo

Makala hii kuhusu mambo ya dini bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu mada hii kama historia yake au uenezi wake?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.