Tunguhina
Tunguhina | ||||||||||||
---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|
Tunguhina kaskazi | ||||||||||||
Uainishaji wa kisayansi | ||||||||||||
| ||||||||||||
Ngazi za chini | ||||||||||||
Spishi 2:
|
Tunguhina ni ndege wadogo wa jenasi Uraeginthus katika familia ya Estrildidae ambao wana rangi kahawianyekundu na viraka buluu au zambarau. Kuna spishi tatu zingine kwa jenasi hii ambazo zinaitwa vitenduli na zina rangi buluu. Wataalamu wengine wanaweka spishi mbili za tunguhina ndani ya jenasi Granatina. Spishi hizi zinatokea Afrika chini ya Sahara tu. Tunguhina ni ndege waoga, lakini kwa bustani ya hoteli na nyumba wanazoea watu. Tago lao hutengenezwa na manyasi ndani ya magugu; limefunikika juu na lina mwingilio kando.
Spishi
- Uraeginthus granatinus, Tunguhina Kusi (Common Grenadier or Violet-eared Waxbill)
- Uraeginthus ianthinogaster, Tunguhina Kaskazi (Purple Grenadier)
Picha
- Tunguhina kusi
- Tunguhina kaskazi
🔥 Top keywords: Maalum:TafutaMwanzoShairiJumuiya ya Afrika MasharikiUfahamu wa uwezo wa kushika mimbaFasihi simuliziNembo ya TanzaniaMshororoMikoa ya TanzaniaVivumishiOrodha ya mikoa ya Tanzania kwa eneoPentekosteAina za manenoTanzaniaKamusi za KiswahiliMfumo wa mmeng'enyo wa chakulaOrodha ya makabila ya TanzaniaAfrika Mashariki 1800-1845Orodha ya Mawaziri Wakuu wa TanzaniaUpendo Furaha PenezaMafurikoMisimu (lugha)KumaKisaweSentensiDiamond PlatnumzKamusi ya Kiswahili sanifuKamusiMisemoMaudhuiSimba S.C.Ukwapi na utaoTanganyikaOrodha ya Watakatifu WakristoNgeliLahaja za KiswahiliMaumivu ya kiunoRoho MtakatifuNomino