Arkadi, Paskasi na wenzao
Arkadi, Paskasi na wenzao Probo, Eutikiani na Paulilo (karibu wote walifariki Afrika Kaskazini, 437) ni kati ya waumini wa Kanisa Katoliki walioteswa kikatili sana na Wavandali katika karne ya 5, wakati wa utawala wa mfalme Genseriki aliyekuwa Mwario.
Wazaliwa wa Hispania, walikuwa askari wa mfalme huyo, Paskasi na Eutikiani walikuwa ndugu na Paulilo alikuwa mdogo wao.
Walipokataa kujiunga na Uario, walifilisishwa, walipelekwa uhamishoni, waliteswa na hatimaye kuuawa, isipokuwa mtoto Paulilo alifanywa mtumwa.
Tangu kale wanaheshimiwa kama watakatifu wafiadini.
Sikukuu yao huadhimishwa tarehe 13 Novemba[1].
Tazama pia
Tanbihi
Makala hii bado ni mbegu. Je, unajua kitu kuhusu Mkristo huyu, kama wasifu wake, habari za maisha au kazi yake? Je, unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa? Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuiongezea habari. |
🔥 Top keywords: Maalum:TafutaMwanzoFasihi simuliziAina za manenoShairiVivumishiMikoa ya TanzaniaOrodha ya makabila ya TanzaniaOrodha ya Mawaziri Wakuu wa TanzaniaUfahamu wa uwezo wa kushika mimbaLughaOrodha ya mikoa ya Tanzania kwa eneoKamusi za KiswahiliMofimuFasihiNembo ya TanzaniaMawasilianoSentensiMarie AntoinetteKamusiMange KimambiKumaViwakilishiAlama ya uakifishajiKitenziFani (fasihi)TamthiliaVitendawiliNominoKiswahiliMaudhuiSilabiTanzaniaJumuiya ya Afrika MasharikiKisaweVieleziYoung Africans S.C.Kiwakilishi nafsiDiamond Platnumz