Wafiadini Wakopti wa Libya
Wafiadini Wakopti wa Libya ni Wakristo 20 wa Kikopti kutoka Misri[1] na Matthew Ayariga kutoka Ghana[2][3][4][5][6][7][8] waliotekwa na Waislamu wenye itikadi kali wa Daish huko Sirte, Libya, walipokuwa wanafanya kazi ya ujenzi tarehe 27 Desemba 2014 na mnamo Januari 2015.[9] Matukio ya dhuluma dhidi ya Wamisri nchini Libya yalianza katika miaka ya 1950.[10]
Hatimaye waliuawa kwa kukatwa kichwa kwa ajili ya imani yao[11][12][13][14][15], kama ilivyoonyeshwa katika video tarehe 15 Februari 2015[16]. Kifo chao kilithibishwa na serikali na Kanisa[17].
Tarehe 21 Februari 2015 Patriarki Tawadros II wa Alexandria aliwatangaza kuwa watakatifu[18]. Papa Fransisko amemuomba ruhusa ya kuwaingiza katika Martyrologium Romanum.
Sikukuu yao huadhimishwa tarehe ya kifodini chao, 15 Februari.
Majina yao
Ni kama ifuatavyo[19][20][21]:
Bishoy Adel Khalaf | Samuel Alhoam Wilson | Hany Abdel-Masih Salib |
Melad Mackeen Zaki | Abanoub Ayad Attia | Ezzat Bushra Nassif |
Yousef Shokry Younan | Kirillos Shukry Fawzy | Majed Suleiman Shehata |
Somali Stéphanos Kamel | Malak Ibrahim Siniot | Bishoy Stéphanos Kamel |
Mena Fayez Aziz | Girgis Melad Sniout | Tawadros Youssef Tawadros |
Essam Badr Samir | Luke Ngati | Jaber Mounir Adly |
Malak Faraj Abram | Sameh Salah Farouk | Matthew Ayariga |
Mwendelezo
Mnamo 19 Aprili 2015, Daish ilisambaza video nyingine iliyoonyesha uuaji wa Wakristo Waethiopia 30 hivi.[22][23][24][25][26][27]
Marejeo
Martin Mosebach aliandika kitabu juu yao: The 21 - A Journey into the Land of Coptic Martyrs.[28]
Tazama pia
Tanbihi
Viungo vya nje
Makala hii bado ni mbegu. Je, unajua kitu kuhusu Mkristo huyu, kama wasifu wake, habari za maisha au kazi yake? Je, unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa? Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuiongezea habari. |