Charles I wa Uingereza
Charles I (19 Novemba 1600 – 30 Januari 1649[1]) alikuwa mfalme wa Uingereza, Uskoti na Ireland kuanzia tarehe 27 Machi 1625 hadi alipouawa.
Alishindana na bunge lililotaka kupunguza mamlaka yake, ambayo mwenyewe alifikiri alipewa na Mungu na anaweza kuitumia kadiri ya dhamiri yake.
Alizidi kuchukiwa kwa kuongeza kodi bila kibali cha bunge, kwa kuoa mwanamke Mkatoliki[2] na kwa kuunga mkono wakleri wenye mwelekeo wa Kikatoliki kama vile Richard Montagu na William Laud, pamoja na kujaribu kulazimisha Kanisa la Uskoti kufuata taratibu za lile la Anglikana.
Hatimaye vita vilizuka dhidi yake, kwanza vita vya Maaskofu, halafu tangu mwaka 1642 Charles alipigana na mabunge ya Uingereza na Uskoti katika vita vya wenyewe kwa wenyewe. Aliposhindwa na kusalimu amri mwaka 1645, alikataa sharti la kukubali ufalme wa kikatiba. Kisha kutoroka mnamo Novemba 1647 alifungwa tena katika kisiwa cha Wight.
Hatimaye, chini ya utawala wa Oliver Cromwell, mnamo Januari 1649 alihukumiwa kuwa msaliti na kupewa adhabu ya kifo[3].
Ufalme ulifutwa ikatangazwa jamhuri (Commonwealth of England). Baadaye (1660) ufalme ulirudishwa chini ya mwanae, Charles II wa Uingereza .
Baadhi ya Waanglikana walimuona kama mfiadini na mwaka 1660 walimuingiza katika kalenda ya watakatifu kwa jina la "Mfalme Charles Mfiadini".
Tazama pia
Tanbihi
Marejeo
- 2013 Check date values in:
|date=, |accessdate=
(help)
Marejeo mengine
- Gardiner, Samuel Rawson (1882), The Fall of the Monarchy of Charles I, 1637–1649: Volume I (1637–1640); Volume II (1640–1642)
Viungo vya nje
- Official website of the British monarchy
- The Society of King Charles the Martyr
- The Society of King Charles the Martyr (United States)
- Works by Charles I, King of England katika Project Gutenberg
Makala hii kuhusu mwanasiasa fulani bado ni mbegu. Je, unajua kitu kuhusu Charles I wa Uingereza kama wasifu wake, habari za maisha au kazi yake? Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa? Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari. |