Didimo Kipofu

Didimo Kipofu (313 hivi - 398 hivi)[1]) alikuwa mwanateolojia maarufu wa Aleksandria (Misri) ambapo aliongoza chuo cha katekesi kwa karibu miaka 50.

Picha takatifu ya Mt. Didimo Kipofu.

Ingawa hakuweza kuona, alikuwa na kumbukumbu kali sana, hata akaweza kumudu fani zinazofaidika sana na matumizi ya macho.

Aliandika vitabu vingi: Ufafanuzi wa Zaburi zote, wa Injili ya Mathayo na wa Injili ya Yohane, kitabu Dhidi ya Waario, na Juu ya Roho Mtakatifu, ambavyo Jeromu alivitafsiri katika Kilatini. Pia aliandika juu ya Isaya, Hosea, Zekaria, Ayubu na mada nyingine nyingi.[2]

Bahati mbaya, kati ya maandishi ya ufafanuzi ya Didimo, yanayofikiriwa kuhusu vitabu vyote vya Biblia ya Kikristo, vimetufikia vipande tu. Hata hivyo vinatosha kushuhudia upana wa ujuzi wake.

Mfuasi wa Origen, alipinga mafundisho ya Ario na ya Wapneumatomaki.[3]

Tazama pia

Tanbihi

Marejeo

  • Ayres, Lewis, DelCogliano, Mark & Radde-Gallwitz, Andrew (2012). Works on the Spirit: St. Athanasius the Great and Didymus the Blind. St. Vladimir's Seminary Press [contains the only English translation of On the Holy Spirit]
  • Hill, RC, trans. (2006). Didymus. Commentary on Zechariah, FC, Washington, DC: Catholic University of America Press. [contains the only English translation of the Commentary on Zechariah]
  • Sozomen, The Ecclesiastical History of Sozomen, comprising a history of the church, from AD323 to AD425. Translated by Chester D. Hartranft. From Nicene and Post-Nicene Fathers, Second Series. Edited by Philip Schaff and Henry Wace. (Buffalo, NY: Christian Literature Publishing Co., 1890), Vol. 2, Book III, chapter 15: Didymus the blind and Aëtius the heretic. Available at s:Nicene and Post-Nicene Fathers: Series II/Volume II/Sozomen/Book III/Chapter 15#cite note-0 or http://www.newadvent.org/fathers/26023.htm.
  • Sozomen; Philostorgius, Saint Photius I (Patriarch of Constantinople) (1855). The ecclesiastical history of Sozomen: comprising a history of the church from A.D. 324 to A.D. 440. Henry G. Bohn. uk. 132. 

Marejeo mengine

  • Gauche, William (1934). Didymus the Blind: An educator of the 4th century. Washington, D. C.: Catholic University of America.
  • Layton, Richard (2004). Didymus the blind and his circle in late-antique Alexandria. Champaign, IL: University of Illinois Press.
  • Weerakkody, D. P. M. (2006). Didymus the Blind: Alexandrian theologian and scholar. In Albrecht, G. (Editor). Encyclopedia of disability. Volume 1, p. 401.
  • Frances Young with Andrew Teal, From Nicaea to Chalcedon: A Guide to the Literature and its Background, (2nd edn, 2010), pp. 91–101
Makala hii bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Mkristo huyu, kama wasifu wake, habari za maisha au kazi yake?
Je, unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuiongezea habari.