Hidulfi

Hidulfi (pia: Hidulf, Hildulf, Hidulfus, Hidulphus, Hiduiphus, Hidulphe, Hydulphe; alifariki 707) alikuwa mmonaki halafu askofu wa 29 wa Trier, leo nchini Ujerumani, kwa miaka mitano. Baadaye aling'atuka na kwenda kuishi upwekeni kwenye milima ya Vosges, leo nchini Ufaransa, ila alifuatwa na wengi akawaanzishia monasteri ya Moyenmoutier akaiongoza hadi kifo chake [1][2].

Orodha ya maaskofu wa Trier.

Tangu zamani anaheshimiwa na Wakatoliki na Waorthodoksi kama mtakatifu.

Sikukuu yake inaadhimishwa kila mwaka tarehe 11 Julai[3][4].

Tazama pia

Tanbihi

Marejeo

  • Olaf Schneider: Erzbischof Hinkmar und die Folgen: Der vierhundertjährige Weg historischer Erinnerungsbilder von Reims nach Trier. Berlin, New York, 2010
Makala hii bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Mkristo huyu, kama wasifu wake, habari za maisha au kazi yake?
Je, unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuiongezea habari.