Isaka wa Ninawi
Isaka wa Ninawi (kwa Kiaramu ܡܪܝ ܐܝܣܚܩ ܕܢܝܢܘ; kwa Kiarabu: إسحاق النينوي Ishak an-Naynuwī; kwa Kigiriki Ἰσαὰκ Σύρος, Isaac Syuros; kwa Kiingereza Isaac of Nineveh[1][2][3]; 613 hivi – 700 hivi) alikuwa mwanateolojia na askofu wa Kanisa la Asiria.
Ni maarufu hasa kwa maandishi yake juu ya maisha ya Kiroho. Yapo hadi leo katika lugha asili ya Kisiria na katika tafsiri za kale za Kigiriki na Kiarabu. Yametumiwa sana na Wakristo wa madhehebu mengine, hasa ya Mashariki.
Tangu kale anaheshimiwa kama mtakatifu, katika Kanisa lake na makanisa ya Waorthodoksi wa Mashariki na Waorthodoksi.
Sikukuu yake huadhimishwa tarehe 28 Januari.
Maisha
Alizaliwa Beth Qatraye, kati ya Mesopotamia na Arabia (Qatar ?)[4][5][6].
Akiwa bado kijana sana alijiunga na monasteri akafanya bidii sana. Akitumia pia maktaba iliyokuwepo, alijipatia sifa upande wa teolojia akaanza kufundisha dini katika eneo lake asili.
Patriarki Georges alipotembelea eneo hilo katikati ya karne ya 7 ili kushiriki sinodi, alimfanya Isaka kuwa askofu wa Ninawi, Assyria, mbali sana, katika Mesopotamia ya Kaskazini.[7].
Majukumu hayo mapya hayakufaa tabia yake, hivyo baada ya miezi 5 alijiuzulu akarudi kusini katika upweke wa Mlima Matout. Huko aliishi miaka mingi akila mikate 3 tu kwa juma pamoja na mboga kidogo.
Hatimaye uzee na upofu vilimlazimisha kurudi monasterini. Huko Shabar alifariki na kuzikwa.
Tazama pia
Tanbihi
Marejeo
- Misemo ya Mababa wa Jangwani (Apophthegmata Patrum) – tafsiri ya W. Ngowi, O.F.M.Cap. – ed. Salvatorianum – Morogoro 2000 –ISBN 0-264-66350-0
Viungo vya nje
- Shughuli au kuhusu Isaka wa Ninawi katika maktaba ya WorldCat catalog
- St Isaac of Nineveh Orthodox Icon and Synaxarion
- A collection of resources on St. Isaac
- "Isaac of Nineveh". Catholic Encyclopedia. New York: Robert Appleton Company. 1913.
- Saint Isaac, the Syrian in orthodoxwiki.com
- Online edition of the Ascetical Homilies
- Saint Isaac of Nineveh Facebook Page, featuring new translations from Syriac and Arabic
Makala hii bado ni mbegu. Je, unajua kitu kuhusu Mkristo huyu, kama wasifu wake, habari za maisha au kazi yake? Je, unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa? Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuiongezea habari. |