Yakobo Do Mai Nam

(Elekezwa kutoka James Nam)

Yakobo Do Mai Nam (1781-1838) alikuwa padri wa Vietnam ambaye, pamoja na mkulima Antoni Nguyen Dich na daktari Mikaeli My Huy Nguyen, alikatwa kichwa baada ya kuteswa sana wakati wa dhuluma ya kaisari Minh Mang[1].

Ni kati ya Wakristo wafiadini wa Vietnam waliouawa kwa ajili ya imani yao huko Vietnam katika karne ya 17, 18 na 19 (16251886).

Wanatajwa pia kama Watakatifu Andrea Dũng-Lạc na wenzake 116.

Kwa nyakati tofauti, Papa Leo XIII, Papa Pius X na Papa Pius XII waliwatangaza kuwa wenye heri, halafu Papa Yohane Paulo II aliwaunganisha katika kuwafanya watakatifu wafiadini tarehe 19 Juni 1988.

Sikukuu yao huadhimishwa kwa pamoja kila tarehe 24 Novemba, lakini ya kwake mwenyewe tarehe 12 Agosti[2].

Tazama pia

Tanbihi

Marejeo

  • Les Missions Etrangères. Trois siecles et demi d'histoire et d'aventure en Asie Editions Perrin, 2008, ISBN 978-2-262-02571-7
  • "St. Andrew Dung-Lac & Martyrs", by Father Robert F. McNamara, Saints Alive and All God's Children Copyright 1980-2010 Rev. Robert F. McNamara and St. Thomas the Apostle Church.
  • "Vietnamese Martyr Teaches Quiet Lessons", By Judy Ball, An AmericanCatholic.org Web Site from the Franciscans and St. Anthony Messenger Press.

Viungo vya nje

WikiMedia Commons
Makala hii bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Mkristo huyu, kama wasifu wake, habari za maisha au kazi yake?
Je, unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuiongezea habari.