Kigunduzi moshi
Zana
Kijumla
Chapa/peleka nje
Miradi mingine
Kigunduzi moshi (kwa Kiingereza: smoke detector) ni kifaa kinachoweza kugundua moshi, ambao unaweza kuwa kiashiria cha moto.
Kuna mifumo miwili ya kimsingi:
Vigunduzi moshi hutumia moja kati ya mifumo miwili kutambua moshi:
Kigunduzi moshi kinuru (optical smoke detector) huwa na kifaa cha kupima mabadiliko ya nuru wakati kuna moshi hewani. Hapo inatumia seli ya umemenuru inayopeka nuru kutoka diodi; moshi unafanywa na vipande vidogo vinavyoathiri kiwango cha nuru kinachofika kwenye seli.[1] Mwanga uliotumiwa unaweza kuwa wa infrared, mwanga unaoonekana, au ultraviolet . Hapo kigunduzi hugundua kuna mwanga mdogo. Chini ya mwangaza fulani, kigunduzi kinawasha king’ora.
Kigunduzi cha ioni (ionization smoke detector) huwa na elementi nururifu ndani yake, kwa kawaida kiasi kidogo cha Ameriki. Vigunduzi hivyo huwa na chemba mbili ndani yake, moja iliyofungwa, nyingine iliyo wazi. Unururifu hutoa mionzi ya alfa inayoziionisha molekuli za hewa ndani ya kigunduzi na umeme unaweza kupita kwenye molekuli hizo. Kama moshi unaingia upande wa chemba iliyo wazi, sehemu za nyembe za alfa zitaathiri punje za moshi hewani badala ya molekuli za hewa. Hivyo volteji ya umeme katika chemba iliyo wazi inaanza kuwa tofauti na volteji katika chemba iliyofungwa. Tofauti hiyo inatambuliwa na kigunduzi na kufanya kiwashe king’ora.
Vigunduzi vya ioni hupatikana kwa bei nafuu kuliko vigunduzi vya nuru lakini husababisha pia king’ora cha uwongo zaidi kuliko vile vya nuru. [2] [3]
Makala hii kuhusu mambo ya teknolojia bado ni mbegu. Je, unajua kitu kuhusu mada hiyo kama historia yake au mahusiano yake na mada nyingine? Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa? Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari. |