Vizole ni ndege wadogo kiasi wa jenasiOnychognathus katika familiaSturnidae. Wanatokea Afrika tu isipokuwa kizole Somali na kizole Arabu ambao wanatokea nchi za kiarabu pia. Wanapenda kuwa kwa makundi. Ndege hawa wana mabawa mekundu yaonekanayo sana wakiruka anwani. Manyoya ya dume ni meusi na yale ya jike yana rangi ya kijivu cheusi. Hula wadudu na matunda hasa, lakini hula nusra kila kitu. Hulijenga tago lao juu ya kipande cha jabali kilichojitokeza nje katika mahali penye kulindwa. Kizole mabawa-mekundu hutaga mijini pia juu ya vishubaka au mahali pengine penye kulindwa. Jike huyataga mayai 2-4 buluu.