Marinus na Asteri

Marinus na Asteri (walifariki Kaisarea Baharini, leo nchini Israeli, 262) walikuwa Wakristo ambao walikatwa kichwa kwa sababu ya imani yao chini ya Kaizari Galienus ingawa yeye alikuwa amesimamishwa dhuluma[1] [2].

Marinus alikuwa akida ambaye aliposhtakiwa na askari mwenzake akaungama wazi imani yake mbele ya hakimu akakatwa kichwa [3]. Basi, Asteri, seneta wa Dola la Roma, alitandaza joho lake chini kupokea maiti kwa heshima; kwa ajili hiyo yeye pia akakatwa kichwa hapohapo.

Tangu kale wanaheshimiwa na Wakatoliki na Waorthodoksi kama watakatifu wafiadini.

Sikukuu yao huadhimishwa tarehe 3 Machi[4][5].

Tazama pia

Tanbihi

Makala hii bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Mkristo huyu, kama wasifu wake, habari za maisha au kazi yake?
Je, unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuiongezea habari.