Martiniani, Saturiani na wenzao
Martiniani, Saturiani na wenzao wawili walikuwa wote ndugu; ni kati ya wafiadini wa Kanisa Katoliki waliouawa kikatili sana na Wavandali katika karne ya 5, wakati wa utawala wa mfalme Genseriki aliyekuwa Mwario.
Wote waliongokea Ukristo kwa njia ya Masima bikira, mtumwa mwenzao.
Baada ya kutoroka, walijiunga na monasteri huko Thabraca, lakini walikamatwa na kuuzwa tena.
Huko walikopelekwa (Caprapicta) walivuta wengi katika Ukristo wa Kikatoliki[1], jambo lililosababisha chuki ya Waario hadi wakauawa pengine pamoja na wenzao 361, wakiwemo Saturnini, Nerei na Serea[2].
Habari zao zimeandikwa na askofu Vikta wa Vita.
Tangu kale wanaheshimiwa kama watakatifu.
Tazama pia
Tanbihi
Makala hii bado ni mbegu. Je, unajua kitu kuhusu Mkristo huyu, kama wasifu wake, habari za maisha au kazi yake? Je, unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa? Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuiongezea habari. |
🔥 Top keywords: Maalum:TafutaMwanzoFasihi simuliziAina za manenoShairiVivumishiMikoa ya TanzaniaOrodha ya makabila ya TanzaniaOrodha ya Mawaziri Wakuu wa TanzaniaUfahamu wa uwezo wa kushika mimbaLughaOrodha ya mikoa ya Tanzania kwa eneoKamusi za KiswahiliMofimuFasihiNembo ya TanzaniaMawasilianoSentensiMarie AntoinetteKamusiMange KimambiKumaViwakilishiAlama ya uakifishajiKitenziFani (fasihi)TamthiliaVitendawiliNominoKiswahiliMaudhuiSilabiTanzaniaJumuiya ya Afrika MasharikiKisaweVieleziYoung Africans S.C.Kiwakilishi nafsiDiamond Platnumz