Ndezi
Ndezi | ||||||||||||||
---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|
Ndezi mkubwa (Thryonomys swinderianus) | ||||||||||||||
Uainishaji wa kisayansi | ||||||||||||||
| ||||||||||||||
Ngazi za chini | ||||||||||||||
Spishi 2:
|
Ndezi ni wagugunaji wakubwa wa familia Thryonomyidae ambao wana mnasaba karibu kiasi na nungunungu. Wanatokea mahali panyevu pa Afrika kusini kwa Sahara. Wamo miongoni mwa wagugunaji kubwa kabisa duniani. Mwili wao una urefu wa sm 35-60 na uzito wa kg 6-10. Wana manyoya magumu yenye rangi ya kahawa na vidoa kijivu na njano. Hula manyasi ya maji porini lakini katika maeneo ya kilimo hula mimea ya shamba kama muwa, muhogo n.k. Wanaweza kudidimiza hasara kubwa. Ndezi hufugwa sana huko Benini na Togo, na hata nchini Kameruni, Kodivaa, Gaboni, Gana, Nijeria, Senegali na Kongo wakulima wahimizwa kufuga wanyama hawa. Nyama yao ni nzuri sana..
Spishi
- Thryonomys gregorianus, Ndezi Mdogo (Lesser Cane Rat)
- Thryonomys swinderianus, Ndezi Mkubwa (Greater Cane Rat)
Picha
- Ndezi waliogwiwa nchini Kodivaa
- Ndezi afugwaye nchini Gaboni
- Ndezi afugwaye nchini Kameruni
🔥 Top keywords: Maalum:TafutaMwanzoShairiJumuiya ya Afrika MasharikiUfahamu wa uwezo wa kushika mimbaFasihi simuliziNembo ya TanzaniaMshororoMikoa ya TanzaniaVivumishiOrodha ya mikoa ya Tanzania kwa eneoPentekosteAina za manenoTanzaniaKamusi za KiswahiliMfumo wa mmeng'enyo wa chakulaOrodha ya makabila ya TanzaniaAfrika Mashariki 1800-1845Orodha ya Mawaziri Wakuu wa TanzaniaUpendo Furaha PenezaMafurikoMisimu (lugha)KumaKisaweSentensiDiamond PlatnumzKamusi ya Kiswahili sanifuKamusiMisemoMaudhuiSimba S.C.Ukwapi na utaoTanganyikaOrodha ya Watakatifu WakristoNgeliLahaja za KiswahiliMaumivu ya kiunoRoho MtakatifuNomino