Ositha

Ositha (pia:Osgyth, Osyth, Sythe na Othith; alifariki 700 hivi) alikuwa binti wa ukoo wa kifalme wa Mercia.

Mchoro mdogo katika "La Vie seinte Osith, virge e martire" (Campsey Manuscript, British Library Additional Ms 70513, fol. 134v).

Mzaliwa wa Quarrendon, Buckinghamshire alilelewa katika monasteri hukon Warwickshire chini ya mtakatifu Modwen akatamani kuwa abesi, lakini alilazimishwa na baba yake Mpagani kuolewa na mfalme Sighere wa Essex akamzalia mtoto wa kiume.

Baadaye akaweka nadhiri za kimonaki akaanzisha monasteri huko Chich, Essex, akaiongoza hadi kifo chake ambacho kilihesabiwa kama kifodini[1].

Tangu kale anaheshimiwa na Wakatoliki na Waanglikana kama mtakatifu.

Sikukuu yake huadhimisha tarehe 7 Oktoba.

Tazama pia

Tanbihi

Marejeo

  • Oxford Dictionary of National Biography
  • Biographical Dictionary of Dark Age Britain.
  • Geoffrey of Burton's life of Modwenna includes material on Osgyth.
  • Bethell's "Lives of St. Osyth of Essex and St. Osyth of Aylesbury", Analecta Bollandiana 88 (1970).
  • Bailey, "Osyth, Frithuwold and Aylesbury" in Records of Buckinghamshire 31 (1989)
  • Hohler, "St Osyth and Aylesbury", Records of Buckinghamshire 18.1 (1966).

Viungo vya nje

Makala hii bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Mkristo huyu, kama wasifu wake, habari za maisha au kazi yake?
Je, unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuiongezea habari.