Papa Sixtus II

(Elekezwa kutoka Papa Sisto II)

Papa Sixtus II alikuwa Papa kuanzia tarehe 30 Agosti 257 hadi kifodini chake tarehe 6 Agosti 258[1]. Alitokea Ugiriki[2].

Kuuawa kwa Papa Sixtus II na mashemasi wake 6.

Alimfuata Papa Stefano I akafuatwa na Papa Dionysius.

Alirudisha umoja na makanisa ya Mashariki na Afrika Kaskazini uliowahi kuhatarishwa na misimamo tofauti kuhusu ubatizo uliotolewa na waliojitenga na Kanisa Katoliki.

Alikamatwa akihubiria ndugu wa imani juu ya sheria za Mungu wakati wa adhimisho la ekaristi[3].

Tangu kale anaheshimiwa kama mtakatifu mfiadini pamoja na mashemasi wake sita: Januari, Vinsenti, Magnus, Stefano, mbali ya Agapito na Felisisimi waliouawa siku hiyohiyo sehemu nyingine chini ya kaisari Valeriani[4]. Katika Kanuni ya Kirumi anatajwa pamoja na shemasi wake wa saba, Laurenti, aliyeuawa siku tatu baadaye.

Sikukuu yake ni tarehe 7 Agosti[5].

Tazama pia

Maandishi yake

Tanbihi

Viungo vya nje

Wikimedia Commons ina media kuhusu:
Makala hii kuhusu Papa fulani bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Papa Sixtus II kama wasifu wake, habari za maisha au kazi yake?
Je, unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuiongezea habari.