Rabanus Maurus
Rabanus Maurus Magnentius (Mainz, 780 hivi – Oestrich-Winkel, 4 Februari 856), alikuwa mmonaki Mbenedikto maarufu kama mwanateolojia na mhubiri, ambaye akawa askofu mkuu wa Mainz, Ujerumani.
Ndiye mtunzi wa kamusi elezo De rerum naturis ("Mambo ya uasilia") na wa vitabu mbalimbali kuhusu malezi, sarufi na ufafanuzi wa Biblia[1].
Kwa umuhimu wake kati ya walimu wa kipindi cha Karolo Mkuu, aliitwa "Praeceptor Germaniae" ("mwalimu wa Ujerumani").
Anasifiwa kwa kutoacha chochote alichoweza kufanya kwa utukufu wa Mungu.
Katika Martyrologium Romanum anatajwa kama mtakatifu wa Kanisa Katoliki, sikukuu yake ikiwa tarehe 4 Februari[2].
Tazama pia
Tanbihi
Marejeo
- "Blessed Maurus Magnentius Rabanus". Catholic Encyclopedia. New York: Robert Appleton Company. 1913.
- Opera Omnia by Migne Patrologia Latina with analytical indexes
Viungo vya nje
Wikimedia Commons ina media kuhusu:
- Veni Creator Spiritus (with phonetic pronunciation)
- Come Holy Ghost, Creator Blest, Ann Blyth
- Pope Benedict XVI, "Rabanus Maurus", General Audience June 3, 2009
Makala hii bado ni mbegu. Je, unajua kitu kuhusu Mkristo huyu, kama wasifu wake, habari za maisha au kazi yake? Je, unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa? Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuiongezea habari. |
🔥 Top keywords: Maalum:TafutaMwanzoFasihi simuliziAina za manenoShairiVivumishiMikoa ya TanzaniaOrodha ya makabila ya TanzaniaOrodha ya Mawaziri Wakuu wa TanzaniaUfahamu wa uwezo wa kushika mimbaLughaOrodha ya mikoa ya Tanzania kwa eneoKamusi za KiswahiliMofimuFasihiNembo ya TanzaniaMawasilianoSentensiMarie AntoinetteKamusiMange KimambiKumaViwakilishiAlama ya uakifishajiKitenziFani (fasihi)TamthiliaVitendawiliNominoKiswahiliMaudhuiSilabiTanzaniaJumuiya ya Afrika MasharikiKisaweVieleziYoung Africans S.C.Kiwakilishi nafsiDiamond Platnumz