Sila
Sila au Siluano (kwa Kigiriki: Σίλας / Σιλουανός; karne ya 1 AD) ni mmojawapo kati ya viongozi muhimu zaidi wa Kanisa la mwanzo huko Yerusalemu[1].
Kutoka huko alitumwa mara nyingi kwa Wakristo wasio Wayahudi kushughulikia matatizo mbalimbali (kuanzia Mdo 15:22) akawa mwenzi wa Mtume Paulo katika safari za kimisionari (kuanzia Mdo 16:25) akatimiza hadi mwisho huduma zake kwa neema ya Mungu na bidii isiyokubali kuchoka.
Anatajwa na Paulo katika barua mbalimbali (k.mf. 2Kor 1:19).
Hatimaye alimsaidia Mtume Petro kuandika waraka yake wa kwanza (1 Pet 5:12).[2]
Anaheshimiwa na madhehebu mengi ya Ukristo kama mtakatifu, ila tarehe ya sikukuu yake ni tofautofauti. Kwa Wakatoliki ni tarehe 13 Julai[3].
Tazama pia
Tanbihi
Makala hii kuhusu mtu wa Biblia bado ni mbegu. Je, unajua kitu kuhusu Sila kama habari za maisha au kazi yake? Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa? Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari. |
🔥 Top keywords: Maalum:TafutaMwanzoFasihi simuliziAina za manenoShairiVivumishiMikoa ya TanzaniaOrodha ya makabila ya TanzaniaOrodha ya Mawaziri Wakuu wa TanzaniaUfahamu wa uwezo wa kushika mimbaLughaOrodha ya mikoa ya Tanzania kwa eneoKamusi za KiswahiliMofimuFasihiNembo ya TanzaniaMawasilianoSentensiMarie AntoinetteKamusiMange KimambiKumaViwakilishiAlama ya uakifishajiKitenziFani (fasihi)TamthiliaVitendawiliNominoKiswahiliMaudhuiSilabiTanzaniaJumuiya ya Afrika MasharikiKisaweVieleziYoung Africans S.C.Kiwakilishi nafsiDiamond Platnumz