Simeoni wa Mnarani Kijana

Simeoni wa Mnarani Kijana (kwa Kiarabu مار سمعان العمودي الأصغر mār semʻān l-ʻamūdī l-asghar; Antiokia, leo nchini Uturuki, 521 - Antiokia, 24 Mei 592) alikuwa mkaapweke aliyepata umaarufu kwa kuishi miaka 68 juu ya minara mbalimbali akianzia utotoni[1] kwa kufuata mfano wa Yohane, kiongozi wake wa kiroho.

Picha takatifu ya Kiorthodoksi ya Mt. Simeoni.

Alipohama mnara mmoja kwenda mwingine alipata nafasi ya kupewa ushemasi halafu upadri.

Mbali na kutenda miujiza mingi, aliacha maandishi mbalimbali[2].

Umeongezewa sifa "kijana" ili kumtofautisha na waliofuata mtindo wake huo kama Simeoni wa Mnarani Mzee, Simeoni wa Mnarani III na Simeoni wa Mnarani wa Lesbos[3].

Tangu kale anaheshimiwa na Waorthodoksi, Waorthodoksi wa Mashariki, Wakatoliki na Waanglikana kama mtakatifu kama mama yake, Marta wa Antiokia.

Sikukuu yake huadhimishwa tarehe 24 Mei [4].

Tazama pia

Tanbihi

Viungo vya nje

WikiMedia Commons
Makala hii bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Mkristo huyu, kama wasifu wake, habari za maisha au kazi yake?
Je, unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuiongezea habari.