Solomoni wa Bretagne

Solomoni III wa Bretagne (kwa Kibretoni: Salaün; alifariki Bretagne, leo nchini Ufaransa, 25 Juni 874) alikuwa mfalme wa Bretagne kuanzia mwaka 857.

Mt. Solomoni III katika mchoro wa ukutani.

Ili kufidia uuaji wa ndugu yake alioufanya kanisani ili kujitwalia madaraka alijitahidi sana kuanzisha majimbo na monasteri na kudumisha haki.

Hatimaye alipofushwa na kuuawa na maadui wake kanisani vilevile[1].

Tangu kale anaheshimiwa na Wakatoliki na Waorthodoksi kama mtakatifu[2].

Sikukuu yake huadhimishwa tarehe ya kifodini chake[3].

Tazama pia

Tanbihi

Makala hii bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Mkristo huyu, kama wasifu wake, habari za maisha au kazi yake?
Je, unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuiongezea habari.