Stefano wa Piperi

Stefano wa Piperi (kwa Kiserbokroatia: Свети Стефан Пиперски; alifariki 20 Mei 1697) alikuwa mmonaki wa Kanisa la Kiorthodoksi la Serbia.

Saint Stephen of Piperi

Anaheshimiwa na Waorthodoksi kama mtakatifu.

Sikukuu yake huadhimishwa tarehe ya kifo chake.[1]

Maisha

Alizaliwa na wazazi fukara wenye imani katika kijiji cha Kuti, huko Župa (Montenegro).

Kisha kujiunga na monasteri ya Morača akawa abati wake.

Waturuki wa Dola la Osmani walipomfukuza, alihamia Rovacki, Turmanj (leo Celište).

Mwaka 1660 alihamia Piperi alipobaki chumbani hadi kifo chake.

Tazama pia

Tanbihi

Makala hii bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Mkristo huyu, kama wasifu wake, habari za maisha au kazi yake?
Je, unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuiongezea habari.