Shesiafu
(Elekezwa kutoka Stizorhina)
Shesiafu | ||||||||||||||
---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|
![]() Shesiafu mwekundu (Stizorhina fraseri) | ||||||||||||||
Uainishaji wa kisayansi | ||||||||||||||
| ||||||||||||||
Ngazi za chini | ||||||||||||||
Jenasi 2:
|
Shesiafu ni ndege wa jenasi Neocossyphus na Stizorhina katika familia ya Turdidae. Ndege hawa ni aina ya mikesha na waitwa pengine jina hili. Wanatokea Afrika tu. Rangi yao kuu ni rangi ya kahawia na kwa kawaida tumbo lao ni jekundu au kahawiachekundu. Hula wadudu hasa lakini wanyama wadogo wengine pia. Mara kwa mara huungana na ndege walawadudu wengine karibu na safu za siafu wakikamata wadudu na wanyama wadogo ambao wanawakimbia siafu. Lakini spishi za Stizorhina hukamata wadudu mara nyingi zaidi kama shore (kwa hivyo jina la kiingereza “Flycatcher-thrush”). Hujenga tago lao kwa umbo wa kikombe mtini. Jike huyataga mayai 2-4.
Spishi
- Neocossyphus rufus, Shesiafu Mkia-mwekundu (Red-tailed Rufous Thrush au Ant-thrush)
- Neocossyphus poensis, Shesiafu Mkia-mweupe (White-tailed Rufous Thrush au Ant-thrush)
- Stizorhina finschi, Shesiafu wa Finsch (Finsch's Rufous Thrush au Finsch's Flycatcher-thrush]])
- Stizorhina fraseri, Shesiafu Mwekundu (Fraser's Rufous Thrush au Rufous Flycatcher-thrush)
🔥 Top keywords: Maalum:TafutaMwanzoShairiJumuiya ya Afrika MasharikiUfahamu wa uwezo wa kushika mimbaFasihi simuliziNembo ya TanzaniaMshororoMikoa ya TanzaniaVivumishiOrodha ya mikoa ya Tanzania kwa eneoPentekosteAina za manenoTanzaniaKamusi za KiswahiliMfumo wa mmeng'enyo wa chakulaOrodha ya makabila ya TanzaniaAfrika Mashariki 1800-1845Orodha ya Mawaziri Wakuu wa TanzaniaUpendo Furaha PenezaMafurikoMisimu (lugha)KumaKisaweSentensiDiamond PlatnumzKamusi ya Kiswahili sanifuKamusiMisemoMaudhuiSimba S.C.Ukwapi na utaoTanganyikaOrodha ya Watakatifu WakristoNgeliLahaja za KiswahiliMaumivu ya kiunoRoho MtakatifuNomino