Vladimir Mkuu
(Elekezwa kutoka Vladimir wa Kiev)
Vladimir Mkuu (958 hivi – 15 Julai 1015) alikuwa mtemi wa Kiev na Novgorod kuanzia mwaka 980 hadi kifo chake.
Mwaka 988 alipokea ubatizo kutoka kwa mapadre wa Kanisa la Bizanti uliofuatwa na ubatizo wa familia na wananchi wa utemi wake aliojitahidi kwa nguvu zote kuwaleta kwenye imani ya Kikristo [1][2].
Tukio hilo liliathiri moja kwa moja utamaduni wa Urusi, Ukraina na Belarus pamoja na historia yote iliyofuata, kwa kuwa Kanisa la Kiorthodoksi liliendelea kuwa dini rasmi katika milki za Kirusi hadi Mapinduzi ya Urusi ya 1917.
Tangu kale anaheshimiwa na Waorthodoksi na Wakatoliki kama mtakatifu.
Tazama pia
Tanbihi
Viungo vya nje
Wikimedia Commons ina media kuhusu:
- Velychenko, Stephen, How Valdamarr Sveinaldsson got to Moscow (krytyka.com), 9 November 2015.
Makala hii bado ni mbegu. Je, unajua kitu kuhusu Mkristo huyu, kama wasifu wake, habari za maisha au kazi yake? Je, unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa? Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuiongezea habari. |
🔥 Top keywords: Maalum:TafutaMwanzoFasihi simuliziAina za manenoShairiVivumishiMikoa ya TanzaniaOrodha ya makabila ya TanzaniaOrodha ya Mawaziri Wakuu wa TanzaniaUfahamu wa uwezo wa kushika mimbaLughaOrodha ya mikoa ya Tanzania kwa eneoKamusi za KiswahiliMofimuFasihiNembo ya TanzaniaMawasilianoSentensiMarie AntoinetteKamusiMange KimambiKumaViwakilishiAlama ya uakifishajiKitenziFani (fasihi)TamthiliaVitendawiliNominoKiswahiliMaudhuiSilabiTanzaniaJumuiya ya Afrika MasharikiKisaweVieleziYoung Africans S.C.Kiwakilishi nafsiDiamond Platnumz