Wiliamu wa Gellone

Wiliamu wa Gellone (au wa Akwitania, au wa Toulouse au wa Orange; kwa Kifaransa: Guillaume; 755 hivi - 28 Mei 812 au 814) alikuwa mtemi wa Toulouse nchini Ufaransa aliyesifiwa na tendi kadhaa kwa uhodari wake vitani[1] dhidi ya Waislamu waliovamia Hispania Kaskazini na Ufaransa Kusini.

Mt. Wiliamu alivyochorwa na Guercino.

Mwaka 804 alianzisha monasteri ya Kibenedikto ambayo miaka miwili baadaye alijiunga nayo hadi kifo chake[2] [3]

Tangu kale anaheshimiwa na Wakatoliki na Waorthodoksi kama mtakatifu. Mwaka 1066 Papa Aleksanda II alithibitisha heshima hiyo.

Sikukuu yake huadhimishwa tarehe 28 Mei[4].

Tazama pia

Tanbihi

Vyanzo

Marejeo mengine

  • Bouchard, Constance Brittain Those of My Blood: Creating Noble Families in Medieval Francia, University of Pennsylvania Press: 2001.
  • René Poupardin, "Ludovico il Pio", cap. XVIII, vol. II (L'espansione islamica e la nascita dell'Europa feudale) della Storia del Mondo Medievale, pp. 558–582.

Viungo vya nje

Wikimedia Commons ina media kuhusu:
Makala hii bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Mkristo huyu, kama wasifu wake, habari za maisha au kazi yake?
Je, unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuiongezea habari.