Lonjino
Zana
Kijumla
Chapa/peleka nje
Miradi mingine
Lonjino (kwa Kilatini Longinus[1]) ni jina linalotumika[2] kwa askari aliyemchoma kwa mkuki Yesu akiwa maiti msalabani kadiri ya Injili ya Yohane 19:34-37[3].
Ingawa Biblia haina habari zaidi juu yake, inasadikika kwamba baadaye akawa Mkristo[4] na pengine hata kwamba akamfia.
Tangu kale anaheshimiwa kama mtakatifu, hasa tarehe 16 Oktoba (Kanisa Katoliki[5], Waorthodoksi na Anglikana), lakini pia tarehe 22 Oktoba au 14 Novemba (Waorthodoksi wa Mashariki) na tarehe nyingine nyingi.
Makala hii kuhusu mtu wa Biblia bado ni mbegu. Je, unajua kitu kuhusu Lonjino kama habari za maisha au kazi yake? Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa? Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari. |