Adiuto wa Cava

Adiuto wa Cava (alifariki karne ya 5) alikuwa askofu wa mji huo wa Italia Kusini lakini alikuwa mzaliwa wa Afrika Kaskazini.

Sanamu yake.

Baada ya kuteswa na Wavandali Waario kwa sababu ya imani yake, alifukuzwa akiwa na wenzake 12, wakiachwa baharini katika meli mbovu isiyoweza kuendeshwa.

Labda wakati huo alikuwa askofu tayari. Baada ya kufika Italia aliongoza jimbo la Cava dei Tirreni.

Tangu kale anaheshimiwa na Wakatoliki na Waorthodoksi kama mtakatifu.

Sikukuu yake huadhimishwa tarehe 1 Septemba.

Tazama pia

Tanbihi

Makala hii bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Mkristo huyu, kama wasifu wake, habari za maisha au kazi yake?
Je, unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuiongezea habari.