Derg
Derg ni neno la Kiethiopia kwa ajili ya "kamati" au "halmashauri". Inamaanisha hasa kikundi cha wanajeshi waliompindua Kaisari Haile Selassie mwaka 1974 na kushika mamlaka ya serikali nchini Ethiopia.
Derg ilikuwa kamati ya wawakilishi kutoka sehemu mbalimbali za jeshi kama jeshi la nchi kavu, wanamaji, wanaanga na polisi. Derg ilitawala hadi 1987.
Kati ya 1975 na 1977 watu makumi elfu waliuawa hovyo kwa amri za Derg.
Mwenyekiti na kiongozi mkuu wa Derg alikuwa Mengistu Haile Mariam.
1987 Derg ilikabidhi madaraka kufuatana na katiba mpya na Ethiopia kutangazwa kuwa jamhuri ya kisoshalisti na Mengistu rais wake.
🔥 Top keywords: Maalum:TafutaMwanzoFasihi simuliziAina za manenoShairiVivumishiMikoa ya TanzaniaOrodha ya makabila ya TanzaniaOrodha ya Mawaziri Wakuu wa TanzaniaUfahamu wa uwezo wa kushika mimbaLughaOrodha ya mikoa ya Tanzania kwa eneoKamusi za KiswahiliMofimuFasihiNembo ya TanzaniaMawasilianoSentensiMarie AntoinetteKamusiMange KimambiKumaViwakilishiAlama ya uakifishajiKitenziFani (fasihi)TamthiliaVitendawiliNominoKiswahiliMaudhuiSilabiTanzaniaJumuiya ya Afrika MasharikiKisaweVieleziYoung Africans S.C.Kiwakilishi nafsiDiamond Platnumz