Felisi wa Gerona

Felisi wa Gerona (alifariki Gerona, leo nchini Hispania, 31 Agosti 304) alikuwa Mkristo kutoka Scillium, Tunisia, aliyekwenda pamoja na shemasi Kukufas kuinjilisha eneo la Katalunya akauawa wakati wa dhuluma ya kaisari Diokletian wa Dola la Roma[1].

Mt. Felisi akiwahubiria wanawake wa Gerona, mchoro wa Jean de Bourgogne (1470-1536).

Tangu kale anaheshimiwa na Wakatoliki na Waorthodoksi kama mtakatifu mfiadini.

Sikukuu yake huadhimishwa tarehe 1 Agosti[2].

Tazama pia

Tanbihi

Makala hii bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Mkristo huyu, kama wasifu wake, habari za maisha au kazi yake?
Je, unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuiongezea habari.