Galilaya
Galilaya (kutoka Kiebrania הגליל (ha-galil), yaani "mzunguko" au "mkoa"; kiasili "galil ha-goyim - mkoa wa wapagani") ni mkoa maarufu kihistoria upande wa kaskazini mwa Israeli au Palestina.
Upande wa mashariki mpaka wake ni mto Yordani, ambao sehemu hiyo unaunda ziwa Genesareti (pia: bahari ya Galilaya).
Waisraeli walipotoka Misri na kuteka nchi ya Kanaani, katika mkoa huo walihamia watu wa makabila ya Dan, Zebuluni, Isakari na Naftali.
Galilaya ndio mkoa ambapo alikulia na kuanza utume wake Yesu, mwanzilishi wa Ukristo.
Kati ya miji na vijiji vya Galilaya vilivyotajwa katika Injili kuna:
- Bethsaida
- Kafarnaumu
- Kana
- Korozain
- Nain
- Nazareti
- Tiberia
🔥 Top keywords: Maalum:TafutaMwanzoFasihi simuliziAina za manenoShairiVivumishiMikoa ya TanzaniaOrodha ya makabila ya TanzaniaOrodha ya Mawaziri Wakuu wa TanzaniaUfahamu wa uwezo wa kushika mimbaLughaOrodha ya mikoa ya Tanzania kwa eneoKamusi za KiswahiliMofimuFasihiNembo ya TanzaniaMawasilianoSentensiMarie AntoinetteKamusiMange KimambiKumaViwakilishiAlama ya uakifishajiKitenziFani (fasihi)TamthiliaVitendawiliNominoKiswahiliMaudhuiSilabiTanzaniaJumuiya ya Afrika MasharikiKisaweVieleziYoung Africans S.C.Kiwakilishi nafsiDiamond Platnumz