SEO

SEO (kifupi cha maneno ya Kiingereza: search engine optimization) ni utaratibu wa kuongeza ubora na wingi wa watembeleaji wa tovuti kwa kuongeza upatikanaji wa tovuti au ukurasa mmojawapo wa tovuti kwa watumiaji wa tovuti za kutafuta kurasa na habari mtandaoni.[1]
Utaratibu huo unajumuisha tu uboreshaji usiotumia malipo ya matangazo.

SEO inaweza kulenga tovuti za kutafuta za aina mbalimbali kama vile utafutaji wa picha, utafutaji wa video, majarida ya kitaaluma, [2] utafutaji wa habari na utafutaji wa kisekta.

Uboreshaji wa tovuti unaweza kujumuisha kuhariri habari zilizomo kwenye tovuti hiyo, kuboresha HTML na mbinu nyingine nyingi. Baadhi ya mbinu zinakubalika na tovuti za kutafuta ile mbinu nyingine huonekana kuwa ni za ulaghai.[3]

Kufikia Mei 2015, utafutaji kwa kutumia simu za mkononi ulipiku ule wa kutumia kompyuta.[4]

Kama mbinu ya kujitangaza mtandaoni, https://ozguraltun.com.tr/ Archived 12 Julai 2013 at the Wayback Machine. inatazama jinsi tovuti za kutafuta zinavyofanya kazi, algorithm zinazoonyesha tabia za tovuti za kutafuta, maneno yanatotumiwa na watafutaji, n.k.

Historia

Waangalizi wa tovuti na watoa habari walianza kuboresha tovuti kwa njia hiyo toka katikati ya 1990. Mwanzoni, waangalizi wa tovuti walitakiwa kutuma anwani za tovuti zao kwa tovuti za kutafuta.[5]

Marejeo

Viungo vya nje


Makala hii kuhusu mambo ya teknolojia bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu mada hiyo kama historia yake au mahusiano yake na mada nyingine?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.