Tabaka (jamii)

Tabaka katika jamii ni kundi la watu linalotofautiana na mengine kwa hali ya elimu, mali au asili. Tofauti kati ya matabaka zinaweza kuwa kubwa mno na kusababisha utovu wa haki.

Matabaka matatu ya Ulaya kabla ya Mapinduzi ya Kifaransa: mkulima akibeba watu wa matabaka ya juu.

Hasa huko India, mtu aliyezaliwa katika tabaka fulani hawezi kupanda chati, hata kama akitajirika, tena watoto wake wataendelea kuhesabiwa wa tabaka hilohilo la mababu wao.

Katika nchi nyingi, matabaka yanategemea hasa uchumi, hivyo kila mtu anaweza kupanda na vilevile kushuka, hata ghafla[1][2].

Pengine wanatofautishwa:

  1. Mabwanyenye, yaani matajiri wa kupindukia
  2. Walala heri, yaani wenye kipato cha kati
  3. Walala hai, yaani wenye chakula cha kutosha, lakini si zaidi
  4. Walala hoi, yaani maskini
  5. Fukara/hohehahe, yaani maskini wa kupindukia

Tanbihi

Marejeo

Viungo vya nje

Wikiquote ina mkusanyiko wa dondoo kuhusu:
Makala hii kuhusu mambo ya uchumi bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Tabaka (jamii) kama historia yake au mahusiano yake na mada nyingine?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.