Ulaya

bara


Ulaya (asili ya jina ni neno la Kiarabu ولاية, wilaayatun[1]; inaitwa pia Uropa) ni bara lenye eneo la km² 10,600,000 tu, lakini wakazi ni milioni 747 [2].

Ulaya kutoka angani.
Ulaya duniani.
Lugha za Ulaya.
Kanda za Ulaya.
Ulaya mwaka 1000 hivi.

Wengi wenye asili ya Ulaya wakati wa ukoloni walitawanyika duniani, hasa Amerika, wakiathiri kote upande wa lugha, utamaduni na dini.

Utawala

Katika karne ya 20, baada ya vita kuu mbili, nchi mbalimbali za Ulaya zilianza kushirikiana kwa njia mbalimbali:

Kanda za Ulaya

Katika orodha inayofuata kanda zinatajwa katika utaratibu wa Umoja wa Mataifa (UN categorisations/map). Lakini utaratibu huo haukubaliki ndani ya Ulaya kwa nchi za Ulaya ya Kati. Wajerumani, Waaustria, Waswisi, Wacheki, Waslovakia na Wapoland hukubaliana ya kwamba wenyewe si Ulaya ya Magharibi wala ya Mashariki ila Ulaya ya Kati. Kuna majadiliano kuhusu mipaka ya kanda hili yasiyokwisha bado, kwa mfano suala la Hungaria au Latvia.

Orodha ya nchi na maeneo

Jina la nchi au eneo,
bendera
Eneo
(km²)
Wakazi
(mnamo Julai 2002 takriban)
Wakazi kwa km²Mji Mkuu

Ulaya ya Mashariki:

Belarus
207,60010,335,38249.8Minsk
Bulgaria
110,9107,621,33768.7Sofia
Ucheki
78,86610,256,760130.1Praha
Hungaria
93,03010,075,034108.3Budapest
Moldova
33,8434,434,547131.0Kishineu
Poland
312,68538,625,478123.5Warshawa
Romania
238,39121,698,18191.0Bukarest
Urusi (2)
3,960,000106,037,14326.8Moscow
Slovakia
48,8455,422,366111.0Bratislava
Ukraine
603,70048,396,47080.2Kiev

Ulaya ya Kaskazini:

Denmark
43,0945,368,854124.6Kopenhagen
Estonia
45,2261,415,68131.3Tallinn
Visiwa vya Faroe (Denmark)
1,39946,01132.9Tórshavn
Finland
337,0305,183,54515.4Helsinki
Guernsey (3)
7864,587828.0St Peter Port
Iceland
103,000279,3842.7Reykjavík
Eire (Ireland )
70,2803,883,15955.3Dublin
Kisiwa cha Man (3)
57273,873129.1Douglas
Jersey (3)
11689,775773.9Saint Helier
Latvia
64,5892,366,51536.6Riga
Lituanya
65,2003,601,13855.2Vilnius
Norwei
324,2204,525,11614.0Oslo
Visiwa vya Svalbard and Jan
Mayen
(Norway)
62,0492,8680.046Longyearbyen
Uswidi
449,9648,876,74419.7Stockholm
Uingereza (Ufalme wa Maungano)
244,82059,778,002244.2London

Ulaya ya Kusini:

Albania
28,7483,544,841123.3Tirana
Andorra
46868,403146.2Andorra la Vella
Bosnia na Herzegovina
51,1293,964,38877.5Sarayevo
Kroatia
56,5424,390,75177.7Zagreb
Gibraltar (Uingereza)
5.927,7144,697.3Gibraltar
Ugiriki
131,94010,645,34380.7Athens
Italia
301,23057,715,625191.6Roma
Masedonia Kaskazini
25,3332,054,80081.1Skopje
Malta
316397,4991,257.9Valletta
Montenegro
316397,4991,257.9Podgorica
Ureno (6)
91,56810,084,245110.1Lisbon
San Marino
6127,730454.6San Marino
Serbia
102,17310,280,000100.6Belgrad
Slovenia
20,2731,932,91795.3Lyublyana
Hispania (7)
498,50640,077,10080.4Madrid
Mji wa Vatikani
0.449002,045.5Mji wa Vatikani

Ulaya ya Magharibi:

Austria
83,8588,169,92997.4Vienna
Ubelgiji
30,51010,274,595336.8Brussels
Ufaransa (8)
547,03059,765,983109.3Paris
Ujerumani (Udachi)
357,02183,251,851233.2Berlin
Liechtenstein
16032,842205.3Vaduz
Luxemburg
2,586448,569173.5Luxemburg
Monako
1.9531,98716,403.6Monako
Uholanzi (9)
41,52616,318,199393.0Amsterdam, Den Haag
Uswisi
41,2907,301,994176.8Bern

Asia ya Magharibi:

Armenia (10)
29,800Yerevan
Azerbaijan (11)
39,7304,198,491105.7Baku
Kupro (12)
5,995780,133130.1Nikosia (Lefkosa)
Georgia (13)}
49,2402,447,17649.7Tbilisi
Uturuki (14)
24,37811,044,932453.1Ankara

Asia ya Kati:

Kazakhstan (15)
370,3731,285,1743.4Astana
Total10,431,299709,022,06168.0

Tanbihi

1. Kanda zinazotajwa (Ulaya ya Kusini – magharibi n.k.) zinafuata utaratibu wa Umoja wa Mataifa UN categorisations/map. Nchi kadhaa zinazotajwa hapo chini zinaweza kuhesabiwa kuwa sehemu ya Ulaya na pia bara nyingine (Asia, Afrika, au Oceania). Hii inategemea na namna ya kugawa kontinenti; pia wakazi wenyewe wanaweza kujielewa tofauti na majirani yao.

2. Urusi ni nchi ya kontinenti mbili za Ulaya ya Mashariki na Asia; namba za wakazi na za eneo zimetasjwa kwa ajili ya sehemu ya Kiulaya pekee.

3–5. Guernsey, Kisiwa cha Man, and Jersey ni maeneo ya kujitegemea chini ya Taji la Ufalme wa Uingereza.

6. Namba za Ureno hazijumlishi Visiwa vya Madeira, ambazo ni sehemu ya Ureno magharibi ya Marokko katika Afrika.

7. Namba za Hispania hazijumlishi Visiwa vya Kanari magharibi ya Marokko katika Afrika, wa maeneo ya Ceuta na Melilla ambayo ni sehemu za Hispania kwenye pwani ya Moroko, Afrika ya Kaskazini.

8. Namba za Ufaransa hazijumlishi maeneo yake yaliyopo Amerika ya Kati au Kusini, Bahari Hindi au Oceania.

9. Uholanzi: Idadi ya wakazi ni ya 2004; Amsterdam ni Mji Mkuu lakini Den Haag ni makao makuuy a serikali.

10. Armenia huhesabiwa mara nyingi kuwa nchi ya kimabara katika Asia ya Magharibi (kufuatana na kanda za UM) na Ulaya ya Mashariki

11. Azerbaijan huhesabiwa mara nyingi kuwa nchi ya kimabara katika Asia ya Magharibi (kufuatana na kanda za UM) na Ulaya ya Mashariki; idadi ya wakazi na eneo zimetajwa za sehemu ya Ulaya pekee.

12. Kupro huhesabiwa mara nyingi kuwa nchi ya kimabara katika Asia ya Magharibi (kufuatana na kanda za UM) na Ulaya ya Kusini; idadi ya wakazi na eneo zimetajwa za sehemu zisozo chini ya Dola ya Kituruki ya Cyprus.

13. Georgia huhesabiwa mara nyingi kuwa nchi ya kimabara katika Asia ya Magharibi (kufuatana na kanda za UM) na Ulaya ya Mashariki; idadi ya wakazi na eneo zimetajwa za sehemu ya Ulaya pekee.

14. Uturuki ni nchi ya kimabara katika Asia ya Magharibi (kufuatana na kanda za UM) na Ulaya ya Kusini; namba zinazotajwa zinahusiana na sehemu ndogo ya Magharibi pakee iliyomo Ulaya hasa jimbo lote la Istanbul.

15. Kazakhstan huhesabiwa mara nyingi kuwa nchi ya kimabara katika Asia ya Magharibi (kufuatana na kanda za UM) na Ulaya ya Mashariki; idadi ya wakazi na eneo zimetajwa za sehemu ya Ulaya pekee.

Tazama pia

Marejeo