Ukuta wa China
Ukuta mkubwa wa China ni kati ya majengo makubwa kabisa yaliyowahi kujengwa duniani. Ni mfululizo wa kuta na ngome unaofuata mpaka kati ya China na mbuga baridi za Asia ya Kaskazini na Asia ya Kati. Ulijengwa kwa shabaha ya kulinda China dhidi ya mashambulio ya makabila ya wahamiaji wa sehemu hizo.
Jumla ya kuta zote ina urefu wa kilomita zaidi ya 21,000. [1][2]
Ujenzi ulianza katika karne ya 7 KK na kuendelea hadi karne ya 16 BK.[3]
Historia ya ukuta
Ukuta ulijengwa na nasaba mbalimbali za watawala wa China tangu mwaka 200 KK. Shabaha yake ilikuwa ulinzi wa milki dhidi ya mataifa na makabila wa kaskazini walioendelea kushambulia China. Watu wa kaskazini walikuwa wahamiaji waliotumia farasi na ngamia, hivyo haikuwa rahisi kujua ni wapi watakapojaribu kuingia.
Ukuta jinsi ulivyo ni ukuta wa nasaba ya Ming uliojengwa kuanzia mnamo mwaka 1500. Mnamo mwaka 1700 ukuta uliachwa bila kutunzwa tena kwa sababu katika karne ya 17 sehemu kubwa za Mongolia nje ya ukuta ziliunganishwa na China.
Vipimo
Ukuta huwa na upana kati ya mita 4 hadi 8 na kimo cha mita 6 hadi 9.
Kila baada ya mita mia minara ilijengwa ukutani. Minara hii ilikuwa vituo vya kulala kwa walinzi, pia ngome zao wakati wa kushambuliwa na vituo vya mawasiliano kati ya mnara na mnara. Kwa jumla ukuta ulikuwa na minara 25,000.
Tanbihi
Viungo vya nje
Makala hii kuhusu maeneo ya China bado ni mbegu. Je unajua kitu kuhusu Ukuta wa China kama historia yake, biashara, taasisi zilizopo, watu au utamaduni? Labda unaona habari katika wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa? Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari. |