Zakaria (Injili)

Zakaria (kwa Kiebrania זכריה, Zekariah; kwa Kigiriki Ζαχαρίας, Zakarias; kwa Kiarabu زَكَرِيَّا, Zakariya; maana yake ni "YHWH amekumbuka") alikuwa kuhani mwaminifu wa Israeli katika karne ya 1 KK. Mke wake aliitwa Elizabeti, naye pia alikuwa wa ukoo wa Haruni.

Mchoro wa karne ya 15 kuhusu Uzazi wa Mt. Yohane Mbatizaji, Elizabeti akiwa upande wa kushoto.
Mt. Zakaria akiandika jina la Mbatizaji kadiri ya Rogier van der Weyden.
Zakaria na Yohane Mbatizaji katika picha ya ukutani ya Kigeorgia iliyoko Yerusalemu.

Hawakupata mtoto hadi uzeeni kutokana na utasa wa mwanamke, lakini hatimaye walijaliwa kumzaa Yohane Mbatizaji.

Wote wanaheshimiwa kama watakatifu. Sikukuu ya wazazi ni tarehe 5 au 23 Septemba[1], kadiri ya madhehebu. Pengine wanaheshimiwa pamoja na mtoto wao tarehe 24 Juni.

Katika Injili

Habari hizo zinapatikana hasa katika Injili ya Luka, sura ya 1 na ya 2. Humo inaelezwa alivyopashwa na malaika Gabrieli kwamba atapata mtoto wa kiume ambaye atakakuwa nabii mkuu na kumtangulia Bwana[2].

Ingawa Zakaria hakusadiki mara, na kwa sababu hiyo aliadhibiwa kwa kufanywa bubu na kiziwi hadi ahadi itimie, siku ya kumtahiri mtoto alifungua tena kinywa chake na kutoa unabii.

Kadiri ya Lk 1:68-79, siku hiyo Zakaria alitunga wimbo ambao ni maarufu kwa jina la neno la kwanza katika tafsiri ya Kilatini, Benedictus (yaani "Asifiwe"). Katika madhehebu mbalimbali ya Ukristo, wimbo huo wa Kiinjili unatumika kila siku katika Masifu ya asubuhi.

Katika Kurani

Hata Kurani inamtaja mara kadhaa kama nabii na mzazi wa nabii Yahya, hasa katika sura ya 3 na ya 19.

Tazama pia

Tanbihi

Viungo vya nje

Wikimedia Commons ina media kuhusu:


Makala hii kuhusu mtu wa Biblia bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Zakaria (Injili) kama habari za maisha au kazi yake?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.