Mkoa wa Tabora

mkoa wa Tanzania


Mkoa wa Tabora ni kati ya mikoa 31 ya Tanzania wenye postikodi namba 45000.

Mkoa wa Tabora
Mahali paMkoa wa Tabora
Mahali paMkoa wa Tabora
Mahali pa Mkoa wa Tabora katika Tanzania
Majiranukta: 5°30′S 32°50′E / 5.500°S 32.833°E / -5.500; 32.833
NchiTanzania
Wilaya8
Mji mkuuTabora
Serikali
 - Mkuu wa MkoaACP Advera John Bulimba
Eneo
 - Jumla76,151 km²
Idadi ya wakazi (2022)
 - Wakazi kwa ujumla 3,391,679
Tovuti:  http://www.tabora.go.tz/

Ramani ya Mkoa wa Tabora na wilaya zake 7.

Tabora wakati wa ukoloni wa Wajerumani.

Makao makuu yako Tabora Mjini. Tabora ni jina la mji, wilaya na mkoa wa Tanzania ya kati.

Eneo la mkoa ni km2 76,151; mnamo km2 34,698 (46%) ni hifadhi ya misitu, km2 17,122 (22%) ni hifadhi ya wanyama.

Jumla ya wakazi ilikuwa watu 3,391,679 (2022[1]). Wenyeji wa Tabora ni hasa Wanyamwezi. Walio wengi ni wakulima na wafugaji.

Kuna wilaya 8 (katika mabano idadi ya wakazi mwaka 2022[2]): Tabora Mjini (308,741), Nzega Vijijini (574,498), Nzega Mjini (125,193), Igunga (546,204), Uyui (562,588), Urambo (260,322), Sikonge (335,686), Kaliua (678,447).

Jina la Urambo humkumbuka Mtemi Mirambo aliyekuwa mtawala muhimu wa Wanyamwezi kabla ya kuingia kwa ukoloni.

Barabara

Mkoa wa Tabora una barabara za lami. Ipo inayoanzia Tabora mjini hadi Nzega kuelekea Mwanza. Pia lami kutoka Nzega kuelekea Igunga mpaka Singida.

Barabara nyingine ya lami ipo inayoanzia Tabora mjini mpaka Urambo yenye urefu wa km 93.

Pia lami nyingine inaanzia Tabora mjini mpaka Manyoni yenye urefu wa km 254 ukipitia Itigi.

Kuna njia ya reli ya kati kutoka Dar es Salaam kwenda Kigoma kwa upande moja na kwenda Mwanza kwa upande mwingine.

Majimbo ya bunge

Wakati wa uchaguzi mkuu wa Tanzania mwaka 2015 mkoa huu ulikuwa na majimbo ya uchaguzi yafuatayo:

  • Bukene:mbunge ni Suleiman Zedi(CCM)
  • Igalula:mbunge ni Ntimizi Rashidi Mussa(CCM))
  • Igunga:mbunge ni Dk. Dalaly Peter Kafumu(CCM)
  • Kaliua:mbunge ni Magdalena Sakaya(CUF)
  • Manonga:mbunge ni Seif Hamis Said Gulamali(CCM)
  • Nzega Mjini:mbunge ni Hussein Bashe(CCM)
  • Nzega Vijijini:mbunge ni Hamis Kigwangallah(CCM)
  • Sikonge:mbunge ni George Kakunda(CCM)
  • Tabora Mjini:mbunge ni Emmanuel Mwakasaka(CCM)
  • Ulyankulu:mbunge ni John Peter Kadutu(CCM)
  • Urambo:mbunge ni Margareth Sitta(CCM)
  • Uyui:mbunge ni Maige Athumani Almas(CCM)

Tazama pia

Tanbihi


Makala hii kuhusu maeneo ya Mkoa wa Tabora bado ni mbegu.
Je unajua kitu kuhusu Mkoa wa Tabora kama historia yake, biashara, taasisi zilizopo, watu au utamaduni?
Labda unaona habari katika wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.
Tafadhali usiingize majina ya maafisa au viongozi wa sasa maana wanabadilika mno.