Papa Boniface I
Papa Boniface I alikuwa Papa kuanzia tarehe 28/29 Desemba 418 hadi kifo chake tarehe 4 Septemba 422[1]. Alitokea Roma, Italia, alipopewa ushemasi na Papa Damaso I.
Alimfuata Papa Zosimus[2] akafuatwa na Papa Selestino I.
Kabla ya kuchaguliwa Papa alikuwa balozi wa Papa Inosenti I huko Konstantinopoli[3].
Kama Papa alijitahidi kurudisha na kudumisha nidhamu ndani ya Kanisa[4] na kutetea mamlaka ya Kanisa la Roma katika Iliriko[5].
Alimuunga mkono Agostino wa Hippo dhidi ya uzushi wa Upelaji[6]
Tangu kale anaheshimiwa kama mtakatifu.
Tazama pia
Maandishi yake
Tanbihi
Marejeo
- Catholic Encyclopedia, Volume II. New York 1907, Robert Appleton Company. * Liber Pontificalis, toleo la Duchesne (Paris, 1886), 1, pp. lxii, 227-229;
- Jaffe, Regesta Romanorum Pontificum (Leipzig, 1885), 1, 51-54;
- Louis-Sébastien Le Nain de Tillemont, Mémoires (Venezia, 1732), XII, 385-407, 666-670;
- Karl Joseph von Hefele, Conciliengeschichte and translation, §§ 120, 122;
- Duchesne, Fastes Episcopaux de l'Ancienne Gaul (Paris, 1894), I 84-109;
- Giovanni Sicari, «Reliquie Insigni e "Corpi Santi" a Roma», 1998.
Viungo vya nje
Wikimedia Commons ina media kuhusu:
Makala hii kuhusu Papa fulani bado ni mbegu. Je, unajua kitu kuhusu Papa Boniface I kama wasifu wake, habari za maisha au kazi yake? Je, unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa? Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuiongezea habari. |
🔥 Top keywords: Maalum:TafutaMwanzoFasihi simuliziAina za manenoShairiVivumishiMikoa ya TanzaniaOrodha ya makabila ya TanzaniaOrodha ya Mawaziri Wakuu wa TanzaniaUfahamu wa uwezo wa kushika mimbaLughaOrodha ya mikoa ya Tanzania kwa eneoKamusi za KiswahiliMofimuFasihiNembo ya TanzaniaMawasilianoSentensiMarie AntoinetteKamusiMange KimambiKumaViwakilishiAlama ya uakifishajiKitenziFani (fasihi)TamthiliaVitendawiliNominoKiswahiliMaudhuiSilabiTanzaniaJumuiya ya Afrika MasharikiKisaweVieleziYoung Africans S.C.Kiwakilishi nafsiDiamond Platnumz