Papa Innocent I

Papa Innocent I alikuwa Papa kuanzia tarehe 22 Desemba 401 hadi kifo chake tarehe 12 Machi 417[1]. Alitokea Albano, Roma, Italia[2].

Mt. Inosenti I.

Jambo la pekee katika historia ya Kanisa[3], alimfuata Papa Anastasio I, aliyemzaa kabla ya kupewa upadrisho, akafuatwa na Papa Zosimus.

Aliimarisha mamlaka ya Kanisa la Roma kwa kuamua kesi nyingi za pande zote mbili za Kanisa[4], Mashariki na Magharibi[5]. Alimtetea Yohane Krisostomo, alimfariji Jeromu na kumkubali Augustino.

Alieneza[6] kanuni ya vitabu rasmi vya Biblia inayolingana na ile itakayopitishwa na Mtaguso wa Trento miaka elfu baadaye[7][8][9].

Tangu kale anaheshimiwa na Wakatoliki na Waorthodoksi kama mtakatifu.

Sikukuu yake ni tarehe 12 Machi[10] au 28 Julai.

Tazama pia

Maandishi yake

Tanbihi

Viungo vya nje

Wikimedia Commons ina media kuhusu:
Makala hii kuhusu Papa fulani bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Papa Innocent I kama wasifu wake, habari za maisha au kazi yake?
Je, unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuiongezea habari.