Prokopi Mkuu

Prokopi Mkuu (Yerusalemu, Palestina, karne ya 3 - Kaisarea Baharini, leo nchini Israeli, 8 Julai 303) alikuwa Mkristo aliyeuawa kwa kukatwa kichwa katika mji huo mara alipoanza kutetea kwa ushujaa imani yake mahakamani mwanzoni mwa dhuluma ya kaisari Diokletian[1].

Picha takatifu ya Mt. Prokopi.

Kabla ya hapo aliishi kwa uadilifu na wema[2], pamoja na kuwa mtaalamu wa falsafa na teolojia[3][4].

Tangu kale anaheshimiwa na Wakatoliki na Waorthodoksi kama mtakatifu mfiadini.

Sikukuu yake huadhimishwa tarehe 8 Julai[5] au 22 Novemba[3][4].

Tazama pia

Tanbihi

Viungo vya nje

Makala hii bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Mkristo huyu, kama wasifu wake, habari za maisha au kazi yake?
Je, unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuiongezea habari.