Seneriko

Seneriko (pia: Cerenico, Cinereo, Serenidus, Cénéré, Sénéré, Sérène, Sérenède; Spoleto, Italia, 600 hivi - Le Mans, Ufaransa, 7 Mei 669 au 680) alikuwa mmonaki shemasi ambaye, baada ya kuhiji kwenye makaburi ya Martino wa Tours na Juliani wa Le Mans, alishika maisha magumu upwekeni; inasemekana akaanzisha monasteri yenye watawa 140[1].

Sanamu ya Mt. Seneriko katika mavazi ya kikardinali.

Inasemekana pia kwamva alipokuwa kijana alifanywa kardinali na Papa Martin I[2] .

Anaheshimiwa na Wakatoliki na Waorthodoksi kama mtakatifu.

Sikukuu yake huadhimishwa tarehe 7 Mei[3].

Tazama pia

Tanbihi

Makala hii bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Mkristo huyu, kama wasifu wake, habari za maisha au kazi yake?
Je, unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuiongezea habari.