Tambazi

Tambazi (ing. oedema, edema) ni maradhi inayosababisha uvimbe kwenye mwili. Inaonekana hasa mkononi, mguuni na tumboni lakini inaweza kutokea pia ndani ya mwili.[1]

Tambazi mguuni - baada ya kuminya ngozi alama inabaki kwa muda

Inapatikana wakati viowevu (majimaji) vinatoka kwenye mishipa midogo mwilini na kukusanyika katika tishu yaani kati ya seli za mwili.[2]

Tambazi ya mapafu (ing. pulmonary edema ) ni mkusanyiko wa majimaji kwenye mapafu[3]. Hali hii ni hatari kwa sababu kiowevu ndani ya mapafu inaleta matata ya kupumua, inapunguza oksijeni inayopatikana mwilini na kama ni nyingi sana inaweza kumwua mtu[4].

Tambazi tumboni huitwa ascites.[5]

Makala hii kuhusu mambo ya biolojia bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Tambazi kama historia yake au mahusiano yake na mada nyingine?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.