Camembert (jibini)
Camembert ni jibini laini kutoka Ufaransa. Asili yake iko katika jimbo la kutoka Normandi) kwenye kijiji cha Camembert.
Jibini hii inatengenezwa kwa maziwa ya ng'ombe isiyochemshwa na kuvu ya Camembert (Penicillium camemberti). Inaiva angalau wiki 3 ikifunikwa na ganda la fuvu kabla ya kufungwa katika karatasi na kuuzwa. Hutengenezwa kwa umbo la donge mviringo zenye takriban gramu 250.
Camembert changa ni gumu kiasi lakini kadri inavyozidi kuiva inalainika na kupata ladha ya pekee. Ikikaa muda mrefu ladhaa inaweza kuwa kali na watu wengine wanaipenda vile lakini wengine huona inanuka.
🔥 Top keywords: Maalum:TafutaMwanzoFasihi simuliziAina za manenoShairiVivumishiMikoa ya TanzaniaOrodha ya makabila ya TanzaniaOrodha ya Mawaziri Wakuu wa TanzaniaUfahamu wa uwezo wa kushika mimbaLughaOrodha ya mikoa ya Tanzania kwa eneoKamusi za KiswahiliMofimuFasihiNembo ya TanzaniaMawasilianoSentensiMarie AntoinetteKamusiMange KimambiKumaViwakilishiAlama ya uakifishajiKitenziFani (fasihi)TamthiliaVitendawiliNominoKiswahiliMaudhuiSilabiTanzaniaJumuiya ya Afrika MasharikiKisaweVieleziYoung Africans S.C.Kiwakilishi nafsiDiamond Platnumz