Emeriko wa Hungaria

Emeriko wa Hungaria (pia: Henricus, Emery, Emerick, Emmerich, Emericus or Americus; kwa Kihungaria: Szent Imre herceg; Székesfehérvár, 1007 hivi – Hegyközszentimre, 2 Septemba 1031) alikuwa mtoto wa mfalme Stefano I wa Hungaria ambaye peke yake alifikia ujana[1].

Mt. Emeriko wa Hungaria.

Emeriko alilelewa kitawa na Mbenedikto Gerard wa Csanád ili amrithi baba yake kama mfalme. Alioa mwaka 1022.[2] Kumbe alifariki wakati wa uwindaji.

Mwaka 1083 Papa Gregori VII alimtangaza mtakatifu.

Sikukuu yake huadhimishwa na Wakatoliki na Waorthodoksi, hasa tarehe 4 Novemba[3], lakini pia 5 Novemba na 4 Septemba.

Tazama pia

Tanbihi

Viungo vya nje

Wikimedia Commons ina media kuhusu:
Makala hii bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Mkristo huyu, kama wasifu wake, habari za maisha au kazi yake?
Je, unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuiongezea habari.