Hedwiga wa Poland
Hedwiga (kwa Kijerumani Hedwig; kwa Kipolandi Jadwiga, linatamkwa jadˈviɡa; Budapest, Hungaria, 1373/1374 - Krakov, Polandi, 17 Julai 1399) alikuwa malkia wa Polandi na Lituania.
Kuanzia mwaka 1384 hadi kifo chake alitawala nchi ya Poland akiitwa 'mfalme' badala ya 'malkia', ili kusisitiza kwamba hakuwa tu mke wa mtawala halisi[1].
Alizaliwa katika ukoo wa Wakapeti wa Anjou, binti wa mwisho wa mfalme Luis I wa Hungaria na Elizabeti wa Bosnia.[2].
Kwa kuolewa na Ladislaus wa Lituania, alimfanya abatizwe akaeneza Ukristo katika nchi hiyo ya Kipagani [3].
Tangu zamani anaheshimiwa na Kanisa Katoliki kama mtakatifu na msimamizi wa kila malkia. Papa Yohane Paulo II ndiye aliyemtangaza rasmi mwenye heri tarehe 8 Agosti 1986 na mtakatifu tarehe 8 Juni 1997.
Picha
- The restoration of the Kraków Academy by Queen Jadwiga.
- Psalms of Queen Jadwiga in three languages (Latin, Polish and German).[5]
- Queen Jadwiga's Cup from the Wawel Cathedral.
- Seal of the Jadwiga of Poland
- Jadwiga and Jagiełło (Jogaila) Monument in Kraków Planty Park.
- A later portrait of Jadwiga by Antoni Piotrowski.
Tazama pia
Tanbihi
Marejeo
- Heinze, Karl (8 Desemba 2003). Baltic Sagas. Virtualbookworm Publishing. ISBN 1-58939-498-4.
- Lukowski, Jerzy; Hubert Zawadzki (20 Septemba 2001). A Concise History of Poland. Cambridge University Press. ISBN 0-521-55917-0.
- Turnbull, Stephen; Richard Hook (30 Mei 2003). Tannenberg 1410. Osprey Publishing. ISBN 1-84176-561-9.
Viungo vya nje
Makala hii bado ni mbegu. Je, unajua kitu kuhusu Mkristo huyu, kama wasifu wake, habari za maisha au kazi yake? Je, unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa? Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuiongezea habari. |